30. Na sisi, kwa nini tumo hatarini kila saa?
31. Naam, ndugu, kwa huku kujisifu kwangu niliko nako juu yenu katika Kristo Yesu Bwana wetu, ninakufa kila siku.
32. Ikiwa, kwa jinsi ya kibinadamu, nalipigana na hayawani wakali kule Efeso, nina faida gani? Wasipofufuliwa wafu, na tule, na tunywe, maana kesho tutakufa.
33. Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema.
34. Tumieni akili kama ipasavyo, wala msitende dhambi; kwa maana wengine hawamjui Mungu. Ninanena hayo niwafedheheshe.
35. Lakini labda mtu atasema, Wafufuliwaje wafu? Nao huja kwa mwili gani?
36. Ewe mpumbavu! Uipandayo haihuiki, isipokufa;