1 Kor. 12:7-11 Swahili Union Version (SUV)

7. Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana.

8. Maana mtu mmoja kwa Roho apewa neno la hekima; na mwingine neno la maarifa, apendavyo Roho yeye yule;

9. mwingine imani katika Roho yeye yule; na mwingine karama za kuponya katika Roho yule mmoja;

10. na mwingine matendo ya miujiza; na mwingine unabii; na mwingine kupambanua roho; mwingine aina za lugha; na mwingine tafsiri za lugha;

11. lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye.

1 Kor. 12