1 Fal. 6:25-31 Swahili Union Version (SUV)

25. Na kerubi la pili lilikuwa mikono kumi; makerubi yote mawili walikuwa ya cheo kimoja na namna moja.

26. Kwenda juu kwake kerubi moja kulikuwa mikono kumi, na kerubi la pili vivyo.

27. Akayaweka hayo makerubi katika nyumba ya ndani; na mabawa ya makerubi yakanyoshwa, bawa la moja likafika ukutani huko, na bawa la kerubi la pili likafika ukutani huko; mabawa yao yakagusana katikati ya nyumba.

28. Akayafunika makerubi kwa dhahabu.

29. Akazinakshi kuta zote za nyumba kwa nakshi za makerubi, na mitende, na maua yaliyofunuka wazi, pande za ndani na nje.

30. Na sakafu ya nyumba akaifunika na dhahabu ndani na nje.

31. Akayafanyia maingilio ya chumba cha ndani milango ya mzeituni; kizingiti na miimo ilikuwa ya pande tano.

1 Fal. 6