13. Nami nitakaa katikati ya wana wa Israeli, wala sitawaacha watu wangu Israeli.
14. Basi Sulemani akaijenga hiyo nyumba akaimaliza.
15. Akazijenga kuta za nyumba ndani kwa mbao za mwerezi; toka sakafu ya nyumba hata boriti za juu, akazifunika ndani kwa mti; akafunika sakafu ya nyumba kwa mbao za mberoshi.