1 Fal. 22:46-49 Swahili Union Version (SUV)

46. Tena mahanithi waliosalia, hao waliosalia siku za Asa baba yake, akawaondoa katika nchi.

47. Wala hapakuwa na mfalme katika Edomu; naibu alikuwa ndiye mfalme.

48. Yehoshafati akafanya merikebu za Tarshishi ziende Ofiri kuchukua dhahabu; walakini hazikuenda; kwa maana merikebu zilivunjika huko Esion-geberi.

49. Ndipo Ahazia mwana wa Ahabu akamwambia Yehoshafati, Watumishi wangu na waende pamoja na watumishi wako merikebuni. Lakini Yehoshafati hakukubali.

1 Fal. 22