Zaburi 9:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Nitakushukuru Mungu kwa moyo wangu wote;nitayasimulia matendo yako yote ya ajabu.

2. Nitafurahi na kushangilia kwa sababu yako;nitaliimbia sifa jina lako, ewe Mungu Mkuu.

3. Wakati ulipotokea, maadui zangu walirudi nyuma,walijikwaa na kuangamia.

4. Umenitetea kuhusu kisa changu cha haki;umeketi katika kiti chako cha enzi,ukatoa hukumu iliyo sawa.

5. Umeyakemea mataifa,umewaangamiza waovu;majina yao umeyafutilia mbali milele.

Zaburi 9