5. basi, adui na anifuatie na kunikamata;ayakanyage maisha yangu;na kuniulia mbali.
6. Inuka ee Mwenyezi-Mungu, kwa hasira yako,uikabili ghadhabu ya maadui zangu.Inuka, ee Mungu wangu,wewe umeamuru haki ifanyike.
7. Uyakusanye mataifa kandokando yako,nawe uyatawale kutoka juu.
8. Wewe, ee Mwenyezi-Mungu, wayahukumu mataifa;unihukumu kadiri ya uadilifu wangu,kulingana na huo unyofu wangu.