Zaburi 7:5-8 Biblia Habari Njema (BHN)

5. basi, adui na anifuatie na kunikamata;ayakanyage maisha yangu;na kuniulia mbali.

6. Inuka ee Mwenyezi-Mungu, kwa hasira yako,uikabili ghadhabu ya maadui zangu.Inuka, ee Mungu wangu,wewe umeamuru haki ifanyike.

7. Uyakusanye mataifa kandokando yako,nawe uyatawale kutoka juu.

8. Wewe, ee Mwenyezi-Mungu, wayahukumu mataifa;unihukumu kadiri ya uadilifu wangu,kulingana na huo unyofu wangu.

Zaburi 7