Zaburi 7:1-8 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu, nakimbilia usalama kwako;uniokoe na wote wanaonidhulumu, unisalimishe.

2. La sivyo, watakuja kunirarua kama simba,wakanivutia mbali, pasiwe na wa kuniokoa.

3. Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu!Kama nimetenda moja ya mambo haya:Kama nimechafua mikono yangu kwa ubaya,

4. kama nimemlipa rafiki yangu mabaya badala ya mema,au nimemshambulia adui yangu bila sababu,

5. basi, adui na anifuatie na kunikamata;ayakanyage maisha yangu;na kuniulia mbali.

6. Inuka ee Mwenyezi-Mungu, kwa hasira yako,uikabili ghadhabu ya maadui zangu.Inuka, ee Mungu wangu,wewe umeamuru haki ifanyike.

7. Uyakusanye mataifa kandokando yako,nawe uyatawale kutoka juu.

8. Wewe, ee Mwenyezi-Mungu, wayahukumu mataifa;unihukumu kadiri ya uadilifu wangu,kulingana na huo unyofu wangu.

Zaburi 7