3. mahangaiko yangu yakaniunguza moyoni.Kadiri nilivyowaza ndivyo nilivyotaabika,kisha maneno haya yakanitoka:
4. “Ee Mwenyezi-Mungu, unijulishe mwisho wangu,siku zangu za kuishi zimenibakia ngapi,nijue yapitavyo kasi maisha yangu!”
5. Kumbe umenipimia maisha mafupi sana!Maisha yangu si kitu mbele yako.Hakika, kila binadamu ni kama pumzi tu!
6. Kweli, kila mtu anapita kama kivuli;jitihada zake zote ni bure tu;anakusanya mali, asijue atakayeipata!
7. Na sasa, ee Bwana, ninatazamia nini?Tumaini langu ni kwako wewe!
8. Uniokoe katika makosa yangu yote;usikubali wapumbavu wanidhihaki.
9. Niko kama bubu, sisemi kitu,kwani wewe ndiwe uliyetenda hayo.
10. Usiniadhibu tena;namalizika kwa mapigo yako.