Zaburi 38:13-17 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Lakini mimi nimekuwa kama kiziwi, sisikii;nimekuwa kama bubu asiyeweza kusema kitu.

14. Naam, nimekuwa kama mtu asiyesikia,kama mtu asiye na chochote cha kujitetea.

15. Lakini ninakutumainia wewe, ee Mwenyezi-Mungu;wewe, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu, ndiwe utakayenijibu.

16. Nakuomba tu maadui wasinisimange,wasione fahari juu ya kuanguka kwangu.

17. Karibu sana nitaanguka;nakabiliwa na maumivu ya daima.

Zaburi 38