13. Lakini mimi nimekuwa kama kiziwi, sisikii;nimekuwa kama bubu asiyeweza kusema kitu.
14. Naam, nimekuwa kama mtu asiyesikia,kama mtu asiye na chochote cha kujitetea.
15. Lakini ninakutumainia wewe, ee Mwenyezi-Mungu;wewe, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu, ndiwe utakayenijibu.
16. Nakuomba tu maadui wasinisimange,wasione fahari juu ya kuanguka kwangu.
17. Karibu sana nitaanguka;nakabiliwa na maumivu ya daima.