Zaburi 38:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Ee Mwenyezi-Mungu, usinikemee kwa hasira yako;usiniadhibu kwa ghadhabu yako.

2. Mishale yako imenichoma;mkono wako umenigandamiza.

3. Hamna mahali nafuu mwilini mwangu,kwa sababu umenikasirikia;hamna penye afya hata mifupani mwangu,kwa sababu ya dhambi yangu.

4. Nimefunikwa kabisa na dhambi zangu,zinanilemea kama mzigo mzito mno kwangu.

Zaburi 38