26. Daima huwapa wengine kwa furaha na kukopesha,na watoto wake ni baraka.
27. Achana na uovu, utende mema,nawe utaishi nchini daima;
28. maana Mwenyezi-Mungu hupenda uadilifu,wala hawaachi waaminifu wake.Huwalinda hao milele;lakini wazawa wa waovu wataangamizwa.
29. Waadilifu wataimiliki nchi,na wataishi humo milele.