Zaburi 37:26-29 Biblia Habari Njema (BHN)

26. Daima huwapa wengine kwa furaha na kukopesha,na watoto wake ni baraka.

27. Achana na uovu, utende mema,nawe utaishi nchini daima;

28. maana Mwenyezi-Mungu hupenda uadilifu,wala hawaachi waaminifu wake.Huwalinda hao milele;lakini wazawa wa waovu wataangamizwa.

29. Waadilifu wataimiliki nchi,na wataishi humo milele.

Zaburi 37