Zaburi 37:21-25 Biblia Habari Njema (BHN)

21. Mtu mwovu hukopa bila kurudisha;lakini mwadilifu hutoa kwa ukarimu.

22. Waliobarikiwa na Mwenyezi-Mungu wataimiliki nchi,lakini waliolaaniwa naye watafutiliwa mbali.

23. Mwenyezi-Mungu huziongoza nyayo za mtu,humlinda yule ampendezaye.

24. Ajapoanguka, haanguki akabaki chini,kwa sababu Mwenyezi-Mungu humtegemeza.

25. Nilikuwa kijana na sasa ni mzee;kamwe sijaona mwadilifu ameachwa na Mungu,au watoto wake wakiombaomba chakula.

Zaburi 37