21. Mtu mwovu hukopa bila kurudisha;lakini mwadilifu hutoa kwa ukarimu.
22. Waliobarikiwa na Mwenyezi-Mungu wataimiliki nchi,lakini waliolaaniwa naye watafutiliwa mbali.
23. Mwenyezi-Mungu huziongoza nyayo za mtu,humlinda yule ampendezaye.
24. Ajapoanguka, haanguki akabaki chini,kwa sababu Mwenyezi-Mungu humtegemeza.
25. Nilikuwa kijana na sasa ni mzee;kamwe sijaona mwadilifu ameachwa na Mungu,au watoto wake wakiombaomba chakula.