Zaburi 37:18-25 Biblia Habari Njema (BHN)

18. Mwenyezi-Mungu hutunza maisha ya watu waaminifu,na urithi wao utadumu milele.

19. Hawataaibika zikifika nyakati mbaya;siku za njaa watakuwa na chakula tele.

20. Lakini waovu wataangamia,maadui za Mwenyezi-Mungu watanyauka kama maua nyikani;naam, watatoweka kama moshi.

21. Mtu mwovu hukopa bila kurudisha;lakini mwadilifu hutoa kwa ukarimu.

22. Waliobarikiwa na Mwenyezi-Mungu wataimiliki nchi,lakini waliolaaniwa naye watafutiliwa mbali.

23. Mwenyezi-Mungu huziongoza nyayo za mtu,humlinda yule ampendezaye.

24. Ajapoanguka, haanguki akabaki chini,kwa sababu Mwenyezi-Mungu humtegemeza.

25. Nilikuwa kijana na sasa ni mzee;kamwe sijaona mwadilifu ameachwa na Mungu,au watoto wake wakiombaomba chakula.

Zaburi 37