Zaburi 36:3-7 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Kila asemacho ni uovu na uongo;ameacha kutumia hekima na kutenda mema.

4. Alalapo huwaza kutenda maovu,hujiweka katika njia isiyo njema,wala haachani na uovu.

5. Fadhili zako ee Mwenyezi-Mungu zaenea hata mbinguni;uaminifu wako wafika mawinguni.

6. Uadilifu wako ni kama milima mikubwa,hukumu zako ni kama vilindi vya bahari.Wewe, ee Mwenyezi-Mungu, wawalinda wanadamu na wanyama

7. Jinsi gani zilivyo bora fadhili zako!Wanadamu hukimbilia kivulini mwa mabawa yako.

Zaburi 36