Zaburi 35:17-20 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Ee Mwenyezi-Mungu, utatazama tu mpaka lini?Uniokoe kutoka kwenye mashambulio yao;uyaokoe maisha yangu na simba hao.

18. Hapo nitakushukuru kati ya kusanyiko kubwa la watu;nitakutukuza kati ya jumuiya kubwa ya watu.

19. Usiwaache maadui hao wabaya wanisimange,hao wanichukiao bure wafurahie mateso yangu.

20. Maneno wasemayo si ya amani,wanazua maneno ya hila dhidi ya wananchi watulivu.

Zaburi 35