Zaburi 34:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Nitamtukuza Mwenyezi-Mungu nyakati zote,sitaacha kamwe kuzitamka sifa zake.

2. Mimi nitaona fahari juu ya Mwenyezi-Mungu,wanyonge wasikie na kufurahi.

3. Mtukuzeni Mwenyezi-Mungu pamoja nami,sote pamoja tulisifu jina lake.

Zaburi 34