11. Mpango wa Mwenyezi-Mungu hudumu milele;maazimio yake yadumu vizazi vyote.
12. Heri taifa ambalo Mungu wake ni Mwenyezi-Mungu;heri wale aliowachagua kuwa watu wake mwenyewe!
13. Mwenyezi-Mungu huangalia chini kutoka mbinguni,na kuwaona wanadamu wote.
14. Kutoka kwenye kiti chake cha enzi,huwaangalia wakazi wote wa dunia.
15. Yeye huunda mioyo ya watu wote,yeye ajua kila kitu wanachofanya.
16. Mfalme hawezi kuokolewa kwa kuwa na jeshi kubwa;wala shujaa hapati ushindi kwa nguvu zake kubwa.
17. Farasi wa vita hafai kitu kwa kupata ushindi;nguvu zake nyingi haziwezi kumwokoa mtu.
18. Mwenyezi-Mungu huwaangalia wale wamchao,watu ambao wanatumainia fadhili zake.