Zaburi 33:1-8 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Shangilieni kwa sababu ya Mwenyezi-Mungu enyi waadilifu!Kumsifu Mungu ni wajibu wa watu wanyofu.

2. Msifuni Mwenyezi-Mungu kwa zeze;mwimbieni kwa kinubi cha nyuzi kumi.

3. Mwimbieni wimbo mpya;pigeni kinubi vizuri na kushangilia.

4. Neno la Mwenyezi-Mungu ni la kweli;na matendo yake yote ni ya kuaminika.

5. Mungu apenda uadilifu na haki,dunia imejaa fadhili za Mwenyezi-Mungu.

6. Mbingu ziliumbwa kwa neno la Mwenyezi-Mungu,na vyote vilivyomo kwa pumzi ya mdomo wake.

7. Alikusanya maji ya bahari kama katika chupa,vilindi vya bahari akavifunga ghalani.

8. Dunia yote na imwogope Mwenyezi-Mungu!Wakazi wote duniani, wamche!

Zaburi 33