Zaburi 24:2-6 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Maana yeye aliweka misingi ya dunia juu ya bahari;aliisimika imara juu ya mito ya maji.

3. Nani atakayepanda mlima wa Mwenyezi-Mungu?Nani atakayekaa katika hekalu lake takatifu?

4. Ni mtu wa matendo mema na moyo safi,asiyeuelekeza moyo wake katika upuuzi,wala kuapa kwa uongo.

5. Mtu huyo atapokea baraka kwa Mwenyezi-Mungu,na haki yake kwa Mungu mwokozi wake.

6. Ndio hali ya kizazi cha watu wamtafutao yeye;naam, watu wamtafutao Mungu wa Yakobo.

Zaburi 24