Zaburi 24:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Dunia na vyote vilivyomo ni vyake Mwenyezi-Mungu;ulimwengu na wote waishio humo ni mali yake.

2. Maana yeye aliweka misingi ya dunia juu ya bahari;aliisimika imara juu ya mito ya maji.

3. Nani atakayepanda mlima wa Mwenyezi-Mungu?Nani atakayekaa katika hekalu lake takatifu?

Zaburi 24