7. Mfalme anamtumainia Mwenyezi-Mungu;kwa fadhili za Mungu Mkuu atakuwa salama.
8. Mkono wako ewe mfalme utawakamata maadui zako wote;mkono wako wa kulia utawakamata wanaokuchukia.
9. Utakapotokea utawaangamiza kama kwa tanuri ya moto.Mwenyezi-Mungu atawamaliza kwa hasira yake,moto utawateketeza kabisa.
10. Utawaangamiza wazawa wao kutoka duniani;watoto wao hawatasalia kati ya binadamu.