44. Mara waliposikia habari zangu walinitii.Wageni walinijia wakinyenyekea.
45. Wageni walikufa moyo;wakaja kutoka ngome zao wakitetemeka.
46. Mwenyezi-Mungu yu hai!Asifiwe mwamba wa usalama wangu;atukuzwe Mungu wa wokovu wangu.
47. Yeye ameniwezesha kulipiza kisasi;na kuyashinda mataifa chini yangu.