Zaburi 18:34-41 Biblia Habari Njema (BHN)

34. Hunifunza kupigana vita,mikono yangu iweze kuvuta upinde wa shaba.

35. Umenipa ngao yako ya kuniokoa;mkono wako wa kulia umenitegemeza;wema wako umenifanikisha.

36. Umenirahisishia njia yangu;wala miguu yangu haikuteleza.

37. Niliwafuatia adui zangu na kuwakamata;sikurudi nyuma mpaka nimewaangamiza.

38. Niliwaangusha chini wasiweze kuinuka tena;walianguka chini ya miguu yangu.

39. Wewe ulinijalia nguvu ya kupigana vita;uliwaporomosha maadui chini yangu.

40. Uliwafanya maadui zangu wakimbie,na wale walionichukia niliwaangamiza.

41. Walipiga yowe lakini hapakuwa na wa kuwaokoa;walimlilia Mwenyezi-Mungu lakini hakuwajibu.

Zaburi 18