Zaburi 16:8-11 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Namweka Mwenyezi-Mungu mbele yangu daima;yuko pamoja nami, wala sitatikisika.

9. Kwa hiyo nitafurahi kwa moyo wote na kushangilia,nami nitakaa salama salimini.

10. Naam wewe hutaiacha nafsi yangu kuzimu,hutaniacha mimi mwaminifu wako nipate kuoza.

11. Wanionesha njia ya kufikia uhai;kuwako kwako kwanijaza furaha kamili,katika mkono wako wa nguvu mna mema ya milele.

Zaburi 16