Zaburi 13:2-6 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Nitakuwa na wasiwasi rohoni hadi lini,na sikitiko moyoni siku hata siku?Hadi lini adui zangu watafurahia taabu zangu?

3. Uniangalie na kunijibu, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu.Uyaangazie macho yangu, nisipatwe na usingizi wa kifo.

4. Usiwaache maadui zangu waseme: “Tumemweza huyu!”Watesi wangu wasije wakafurahia kuanguka kwangu.

5. Lakini mimi nazitumainia fadhili zako;moyo wangu na ufurahie wokovu wako.

6. Nitakuimbia wewe, ee Mwenyezi-Mungu,kwa ukarimu mwingi ulionitendea!

Zaburi 13