Yoshua 19:28-32 Biblia Habari Njema (BHN)

28. Ebroni, Rehobu, Hamoni, Kana hadi Sidoni Kuu.

29. Hapo, mpaka uligeuka kuelekea Rama na kufikia kwenye mji wa Tiro uliokuwa na ngome. Kisha ukageuka kuelekea Hosa na kuishia kwenye bahari ya Mediteranea. Miji mingine iliyokuwamo ni Maharabu, Akzibu,

30. Uma, Afeka na Rehobu. Jumla ya miji waliyopewa ni ishirini na miwili pamoja na vijiji vyake.

31. Sehemu hizo ndizo zilizopewa koo za kabila la Asheri; miji hiyo pamoja na vijiji vyake.

32. Kura ya sita ilizipata koo za kabila la Naftali.

Yoshua 19