20. Mto Yordani ndio uliokuwa mpaka wake upande wa mashariki. Ndivyo zilivyowekewa mipaka nchi zilizopewa koo za kabila la Benyamini.
21. Miji ya koo za kabila la Benyamini ni Yeriko, Beth-hogla, Emek-kesisi,
22. Beth-araba, Zemaraimu, Betheli,
23. Avimu, Para, Ofra,
24. Kefar-amoni, Ofni na Geba. Jumla ya miji waliyopewa ni kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.
25. Miji mingine ni Gibeoni, Rama, Beerothi,
26. Mizpa, Kefira, Moza,
27. Rekemu, Irpeeli, Tarala,
28. Zela, Ha-elefu, Yebusi, yaani Yerusalemu, Gibea na Kiriath-yearimu. Jumla ya miji waliyopewa ni kumi na minne pamoja na vijiji vyake. Hiyo yote ni sehemu waliyopewa watu wa kabila la Benyamini na koo zao.