Yohane 9:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Yesu alipokuwa akipita alimwona mtu mmoja, kipofu tangu kuzaliwa.

2. Basi, wanafunzi wakamwuliza, “Mwalimu! Ni nani aliyetenda dhambi: Mtu huyu, ama wazazi wake, hata akazaliwa kipofu?”

3. Yesu akajibu, “Jambo hili halikutukia kwa sababu ya dhambi zake yeye, wala dhambi za wazazi wake; ila alizaliwa kipofu ili nguvu ya Mungu ionekane ikifanya kazi ndani yake.

4. Kukiwa bado mchana yatupasa kuendelea kufanya kazi za yule aliyenituma; maana usiku unakuja ambapo mtu hawezi kufanya kazi.

5. Wakati ningali ulimwenguni, mimi ni mwanga wa ulimwengu.”

Yohane 9