40. Wasamaria walimwendea Yesu wakamwomba akae nao; naye akakaa hapo siku mbili.
41. Watu wengi zaidi waliamini kwa sababu ya ujumbe wake.
42. Wakamwambia yule mama, “Sisi hatuamini tu kwa sababu ya maneno yako; sisi wenyewe tumesikia, na tunajua kwamba huyu ndiye kweli Mwokozi wa ulimwengu.”
43. Baada ya siku mbili Yesu aliondoka hapo, akaenda Galilaya.