8. Naye atakapokuja atawathibitishia walimwengu kwamba wamekosea kuhusu dhambi, uadilifu na hukumu ya Mungu.
9. Wamekosea kuhusu dhambi kwa sababu hawaniamini;
10. kuhusu uadilifu, kwa sababu nakwenda zangu kwa Baba, nanyi hamtaniona tena;
11. kuhusu hukumu, kwa sababu mkuu wa ulimwengu huu amekwisha hukumiwa.
12. “Ninayo bado mengi ya kuwaambieni, ila kwa sasa hamwezi kuyastahimili.