11. Mnapaswa kuniamini ninaposema kwamba mimi niko ndani ya Baba naye Baba yuko ndani yangu. Ama sivyo, aminini kwa sababu ya mambo ninayofanya.
12. Kweli nawaambieni, anayeniamini atafanya mambo ninayofanya mimi; naam, atafanya hata makuu zaidi, kwani ninakwenda kwa Baba.
13. Na chochote mtakachoomba kwa jina langu nitafanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana.
14. Mkiniomba chochote kwa jina langu, nitawafanyieni.
15. “Mkinipenda mtazishika amri zangu.
16. Nami nitamwomba Baba naye atawapeni Msaidizi mwingine, atakayekaa nanyi milele.