Yobu 9:4-10 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Yeye ni mwenye hekima mno na nguvu nyingi,nani aliyepingana naye, akashinda?

5. Yeye huiondoa milima bila yenyewe kutambua,huibomolea mbali kwa hasira yake.

6. Yeye huitikisa dunia kutoka mahali pake,na nguzo zake zikatetemeka.

7. Huliamuru jua lisichomozehuziziba nyota zisiangaze.

8. Yeye peke yake alizitandaza mbingu,na kuyakanyaga mawimbi ya bahari.

9. Ndiye aliyezifanya nyota angani:Dubu, Orioni, Kilimia, na nyota za kusini.

10. Ndiye atendaye makuu yasiyoeleweka,mambo ya ajabu yasiyo na idadi.

Yobu 9