1. Yobu akamjibu Elifazi:
2. “Laiti mahangaiko yangu yangepimwa uzani wake,mateso yangu yote yakawekwa katika mizani!
3. Yangekuwa mazito kuliko mchanga wa pwani.Ndio maana maneno yangu ni ya kuropoka!
4. Naam, mishale ya Mungu Mwenye Nguvu imenichoma;nafsi yangu imekunywa sumu yake.Vitisho vya Mungu vimenikabili.
5. Je, pundamwitu hulia akiwa na majani,au ng'ombe akiwa na malisho?