18. Kwani yeye huumiza na pia huuguza;hujeruhi, na kwa mkono wake huponya.
19. Atakuokoa katika maafa zaidi ya mara moja;katika balaa la mwisho, uovu hautakugusa.
20. Wakati wa njaa atakuokoa na kifo,katika mapigano makali atakuokoa.
21. Utakingwa salama na mashambulio ya ulimi,wala hutaogopa maangamizi yajapo.
22. Maangamizi na njaa vijapo, utacheka,wala hutawaogopa wanyama wakali wa nchi.