Yobu 41:17-20 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Linapoinuka, mashujaa hushikwa na woga,kwa pigo moja huwa wamezirai.

18. Hakuna upanga uwezao kulijeruhi,wala mkuki, mshale au fumo.

19. Kwake chuma ni laini kama unyasi,na shaba kama mti uliooza.

20. Mshale hauwezi kulifanya likimbie;akitupiwa mawe ya teo huyaona kama makapi.

Yobu 41