Yobu 40:10-15 Biblia Habari Njema (BHN)

10. “Basi, jioneshe kuwa na fahari na ukuu,ujipambe kwa utukufu na fahari.

11. Wamwagie watu hasira yako kuu;mwangalie kila mwenye kiburi na kumwangusha.

12. Mwangalie kila mwenye kiburi na kumporomosha,uwakanyage waovu mahali walipo.

13. Wazike wote pamoja ardhini;mfunge kila mmoja kwa kifungo cha kifo.

14. Hapo nitakutambua,kwamba nguvu yako mwenyewe imekupa ushindi.

15. “Liangalie lile dude Behemothi,nililoliumba kama nilivyokuumba wewe.Hilo hula nyasi kama ng'ombe,

Yobu 40