10. “Basi, jioneshe kuwa na fahari na ukuu,ujipambe kwa utukufu na fahari.
11. Wamwagie watu hasira yako kuu;mwangalie kila mwenye kiburi na kumwangusha.
12. Mwangalie kila mwenye kiburi na kumporomosha,uwakanyage waovu mahali walipo.
13. Wazike wote pamoja ardhini;mfunge kila mmoja kwa kifungo cha kifo.
14. Hapo nitakutambua,kwamba nguvu yako mwenyewe imekupa ushindi.
15. “Liangalie lile dude Behemothi,nililoliumba kama nilivyokuumba wewe.Hilo hula nyasi kama ng'ombe,