Yobu 4:9-11 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Mungu huwaangamiza hao kwa pumzi yake,hao huteketezwa kwa pigo la hasira yake.

10. Waovu hunguruma kama simba mkali,lakini meno yao huvunjwa.

11. Simba mwenye nguvu hufa kwa kukosa mawindo,na watoto wa simba jike hutawanywa!

Yobu 4