Yobu 4:18-21 Biblia Habari Njema (BHN)

18. Hata watumishi wake, Mungu hana imani nao;na malaika wake huwaona wana kosa;

19. sembuse binadamu viumbe vya udongo,watu ambao chanzo chao ni mavumbi,ambao waweza kupondwapondwa kama nondo!

20. Binadamu kwa masaa machache tu waweza kuangamia;huangamia milele bila kuacha hata alama yao!

21. Iwapo uzi unaoshikilia uhai wao ukikatwawao hufa tena bila kuwa na hekima.

Yobu 4