11. Simba mwenye nguvu hufa kwa kukosa mawindo,na watoto wa simba jike hutawanywa!
12. “Siku moja, niliambiwa neno kwa siri,sikio langu lilisikia mnongono wake.
13. Nikiwa katika mawazo ya njozi za usiku,wakati usingizi mzito huwashika watu,
14. nilishikwa na hofu na kutetemeka,mifupa yangu yote ikagonganagongana.
15. Upepo ukapita mbele ya uso wangu,nywele za mwilini mwangu zikajisimamisha.
16. Kitu kilisimama tuli mbele yangu,nilipokitazama sikukitambua kabisa.Kulikuwa na umbo fulani mbele yangu;kulikuwa kimya, kisha nikasikia sauti.
17. Binadamu afaye aweza kuwa mwadilifu mbele ya Mungu?Mtu aweza kuwa safi mbele ya Muumba wake?