Yobu 36:6-11 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Hawaachi waovu waendelee kuishi;lakini huwapatia wanaodhulumiwa haki zao.

7. Haachi kuwalinda watu waadilifu;huwatawaza, wakatawala na kutukuka.

8. Lakini kama watu wamefungwa minyororo,wamenaswa katika kamba za mateso,

9. Mungu huwaonesha matendo yao maovu,na kwamba wao ni watu wenye kiburi.

10. Huwafungua masikio wasikie mafunzo,na kuwaamuru warudi na kuacha uovu.

11. Wakimtii Mungu na kumtumikia,hufanikiwa katika siku zao zote;miaka yao yote huwa ya furaha.

Yobu 36