Yobu 36:1-8 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kisha Elihu akaendelea kusema:

2. “Nivumilie kidogo, nami nitakuonesha kitu;maana bado ninacho cha kusema kwa niaba ya Mungu.

3. Nitaleta hekima yangu kutoka mbali sana,na kuonesha kwamba Muumba wangu ni mwadilifu.

4. Kweli maneno yangu si ya uongo;mwenye elimu kamili yuko hapa nawe.

5. “Sikiliza Mungu ni mwenye nguvuwala hamdharau mtu yeyote;uwezo wa akili yake ni mkuu mno!

6. Hawaachi waovu waendelee kuishi;lakini huwapatia wanaodhulumiwa haki zao.

7. Haachi kuwalinda watu waadilifu;huwatawaza, wakatawala na kutukuka.

8. Lakini kama watu wamefungwa minyororo,wamenaswa katika kamba za mateso,

Yobu 36