1. Kisha Elihu akaendelea kusema:
2. “Nivumilie kidogo, nami nitakuonesha kitu;maana bado ninacho cha kusema kwa niaba ya Mungu.
3. Nitaleta hekima yangu kutoka mbali sana,na kuonesha kwamba Muumba wangu ni mwadilifu.
4. Kweli maneno yangu si ya uongo;mwenye elimu kamili yuko hapa nawe.
5. “Sikiliza Mungu ni mwenye nguvuwala hamdharau mtu yeyote;uwezo wa akili yake ni mkuu mno!
6. Hawaachi waovu waendelee kuishi;lakini huwapatia wanaodhulumiwa haki zao.
7. Haachi kuwalinda watu waadilifu;huwatawaza, wakatawala na kutukuka.
8. Lakini kama watu wamefungwa minyororo,wamenaswa katika kamba za mateso,