Yobu 34:20-25 Biblia Habari Njema (BHN)

20. Kufumba na kufumbua hao wamekufa;hutikiswa usiku na kuaga dunia;nao wenye nguvu hufutiliwa mbali bila kutumia nguvu za mtu.

21. “Macho ya Mungu huchunguza mienendo ya watu;yeye huziona hatua zao zote.

22. Hakuna weusi wala giza neneambamo watenda maovu waweza kujificha.

23. Mungu hahitaji kumjulisha mtuwakati wa kumleta mbele ya mahakama yake.

24. Huwaangamiza wenye nguvu bila uchunguzi,na kuwaweka wengine mahali pao.

25. Kwa kuwa anayajua matendo yao yote,huwaporomosha usiku wakaangamia.

Yobu 34