Yobu 32:13-18 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Jihadharini msije mkasema, ‘Sasa tumepata hekima.Atakayemshinda ni Mungu, sio binadamu.’

14. Maneno ya Yobu hayakuwa kwa ajili yangu,kwa hiyo sitamjibu kama mlivyomjibu nyinyi.

15. “Nyinyi mmeduwaa; mmeshindwa,nyinyi hamna cha kusema zaidi.

16. Je, ningoje tu kwa vile hamsemi,kwa sababu mnakaa tu bila kujibu kitu?

17. Mimi pia nitatoa jibu langu;mimi nitatoa pia maoni yangu.

18. Ninayo maneno mengi sana,roho yangu yanisukuma kusema.

Yobu 32