13. Jihadharini msije mkasema, ‘Sasa tumepata hekima.Atakayemshinda ni Mungu, sio binadamu.’
14. Maneno ya Yobu hayakuwa kwa ajili yangu,kwa hiyo sitamjibu kama mlivyomjibu nyinyi.
15. “Nyinyi mmeduwaa; mmeshindwa,nyinyi hamna cha kusema zaidi.
16. Je, ningoje tu kwa vile hamsemi,kwa sababu mnakaa tu bila kujibu kitu?
17. Mimi pia nitatoa jibu langu;mimi nitatoa pia maoni yangu.
18. Ninayo maneno mengi sana,roho yangu yanisukuma kusema.