Yobu 31:10-14 Biblia Habari Njema (BHN)

10. basi, mke wangu na ampikie mume mwingine,na wanaume wengine wamtumie.

11. Jambo hilo ni kosa kuu la jinai,uovu ambao hakimu lazima atoe adhabu.

12. Kosa langu lingekuwa kama moto,wa kuniteketeza na kuangamiza,na kuchoma kabisa mapato yangu yote.

13. Kama nimekataa kesi ya mtumishi wanguwa kiume au wa kike,waliponiletea malalamiko yao,

14. nitafanya nini basi Mungu atakaponikabili?Je, akinichunguza nitamjibu nini?

Yobu 31