Yobu 3:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Hatimaye Yobu aliamua kuongea, akailaani siku aliyozaliwa.

2. Yobu akasema:

3. “Ilaaniwe siku ile niliyozaliwa;usiku ule iliposemwa, ‘Mwana amechukuliwa mimba’

4. Siku hiyo na iwe giza!Mungu juu asijishughulishe nayo!Wala nuru yoyote isiiangaze!

5. Mauzauza na giza nene yaikumbe,mawingu mazito yaifunike.Giza la mchana liitishe!

Yobu 3