Yobu 28:25-28 Biblia Habari Njema (BHN)

25. Alipoupa upepo uzito wake,na kuyapimia maji mipaka yake;

26. alipoamua mvua inyeshe wapi,umeme na radi vipite wapi;

27. hapo ndipo alipoiona hekima na kuitangaza,aliisimika na kuichunguza.”

28. Kisha Mungu akamwambia mwanadamu:“Tazama! Kumcha Bwana ndio hekima;na kujitenga na uovu ndio maarifa.”

Yobu 28