7. Umewanyima maji wale waliokuwa wamechoka;umewanyima chakula wale walio na njaa.
8. Umemruhusu mwenye cheo kuchukua ardhi yote;umemwacha anayependelewa aishi humo.
9. Umewaacha wajane waende mikono mitupu;umewanyima yatima uwezo wao.
10. Kwa hiyo mitego imekuzunguka pande zote,hofu ya ghafla imekuvamia.
11. Giza limekuangukia usione kitu;mafuriko ya maji yamekufunika.
12. Twajua Mungu yuko huko juu mbinguni.Tazama nyota za juu kabisa zilivyo mbali!
13. Lakini wewe wasema: ‘Mungu ajua nini?Je, aweza kupenya mawingu akatoa hukumu?