Yobu 22:24-30 Biblia Habari Njema (BHN)

24. ukitupilia mbali mali yako,ukaitupa dhahabu ya Ofiri ukingoni mwa kijito,

25. Mungu Mwenye Nguvu akawa ndio dhahabu yako,na fedha yako ya thamani;

26. basi, ndipo utakapomfurahia Mungu mwenye nguvuna kutazama kwa matumaini;

27. utamwomba naye atakusikiliza,nawe utazitimiza nadhiri zako.

28. Chochote utakachoamua kitafanikiwa,na mwanga utaziangazia njia zako.

29. Maana, Mungu huwaporomosha wenye majivuno,lakini huwaokoa wanyenyekevu.

30. Yeye humwokoa mtu asiye na hatia;wewe utaokolewa kwa matendo yako mema.”

Yobu 22