Yobu 21:6-12 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Nikifikiri yaliyonipata nafadhaikanafa ganzi mwilini kwa hofu.

7. Kwa nini basi waovu wanaishi bado?Mbona nguvu zao zaongezeka hata uzeeni?

8. Huwaona watoto wao wakifanikiwa;na wazawa wao wakipata nguvu.

9. Kwao kila kitu ni salama bila hofu;wala kiboko cha Mungu hakiwafikii.

10. Naam, ng'ombe wao wote huongezeka,huzaa bila matatizo yoyote.

11. Watoto wao wachanga huwatembeza kama kundi;na watoto wao hucheza ngoma;

12. hucheza muziki wa ngoma na vinubi,na kufurahia sauti ya filimbi.

Yobu 21